Wednesday, April 20, 2011

MAJAMBAZI YAKAMATWA JIJINI MWANZA

 Jana majira ya saa kumi na dakika kadhaa jioni jeshi la polisi mkoani Mwanza limefanikiwa kuwatia nguvuni watu wanne wanaotuhumiwa kwa kufanya ujambazi wakiwa na bunduki moja aina ya smg na bastola mbili moja ikiwa na risasi 12 na na ya pili ikiwa na risasi 2. Kwa mujibu wa kamanda wa jeshi la polisi Mwanza Simon Sirro amesema kuwa watu hao wamekematwa katika eneo la mtaa wa libert jirani na benki ya NMB wakiwa kwenye harakati za safari kuelekea Nyegezi ambako walipanga kwenda kufanya uvamizi kwenye duka moja.
 BASTOLA ZILIZOKAMATWA.
Awali majambazi hayo yalivamia bar moja eneo la kilimahewa na kuwalaza watu chini kisha kupora mali zao na kuiba bastola ya mteja mmoja. Majambazi hayo yaliyokuwa katika gari dogo yalipostukia kuwa yanafuatiliwa yalianza kufyatua risasi hovyo hali iliyosababisha shughuli za biashara kwenye eneo la tukio kusimama kwa muda.
 RISASI 14.
Raia wema ndiyo waliofanikisha kukamatwa kwa majambazi hao kwa kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambao nao bila ajizi walifuatilia nyendo za majambazi hao na hatimaye kufanikiwa kuwatia nguvuni.Wawili kati ya majambazi hayo manne hali zao ni mbaya na wamepelekwa hospitali ya Rufaa Bugando, mmoja katwangwa risasi mguuni na takoni ile hali mwingine sugu anayetambulika kwa jina maarufu 'Askofu' akiwa amevunjika mguu kabisa kwa kutwangwa risasi wakati alipojaribu kuitoroka mikono ya polisi.

Jeshi la polisi mwanza linaendelea kufanya uchunguzi zaidi juu ya tukio zima ambamba na kuwahoji watuhumiwa wote wanne wa mkasa huo.

Saturday, April 16, 2011

Leo ni HEPI BESIDEI YANGU!!!

                                                      Thanks all !!!!! Karibu kwa pilau

Monday, April 11, 2011

Safu ya CCM hii hapa! Lowasa, Chenge, Rostam hawamo! Tafsiri yake nini?

Katibu Mkuu- Wilson Mukama
Naibu Katibu Mkuu (Bara) John Chiligati
Naibu Katibu Mkuu (Visiwani) -Vuai Ali Vuai
Katibu Mwenezi- Nape Nauye
Mambo ya Nje –Januari Makamba
Organaizesheni – Asha Abdala Juma
Uchumi na Fedha -Mwigulu Nchemba

WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU
Anna Abdalah
Peter Kisumo
Mwigulu Nchemba
Januari Makamba
Aly Juma Shamhuna
Wilson Mukama
Emmanuel Nchimbi.

WANAOINGIA KAMATI KUU
Pindi Chana
Abdulrahman Kinana
Zakhia Hamdan Meghji
Abdalah Kigoda
Steven Wasira
Costansia Buhiye
William Lukuvi
Dk. Hussein Ali Mwinyi
Dk. Maua Daftari
Samia Suluhu
Shanmsi Vuai Nahodha
Omary Yusuf Mzee
Prof. Makame Mbarawa
Mohamed Seif Khatibu